UINJILISHAJI MPYA CST
Masista pamoja na kikundi cha WAMISTE (Walei Wamisionari Wateresina)Ni tawi jipya lililoanzishwa na Wateresina kwa lengo la kushiriki katika kazi ya
uinjilishaji wakifuata roho ndogo ya Mtakatifu Teresia wa Mtoto Yesu. Wanainjilisha wakiwa kwenye mazingira yao kufuatana na kazi zao
ili kukoleza roho ya Imani kati ya watu wa Taifa la Mungu. Kwa sasa kikundi hiki kipo katika malezi na wana mikutano yao mara kwa
mara Tosamaganga. Wenye wito wa kujiunga Karibuni. mpate maelezo Tosamaganga Nyumba Asili ya Masista Wateresina.